Tuesday, 23 February 2016

YOU WANT TO SHARE YOUR TESTIMONY? THIS IS HOW TO....


                      6 Points To Note When Giving Testimonies


1. Kabla hujaanza, piga sala- Pray before you begin. Kuomba ni kuzungumza na Mungu, kabala hujafanya chochote, mhusishe yeye Muumba wa vyote.

2. Eleza shida/dhambi yako- Talk your sin. Wafanye wanaokusikiliza ama kukutazama waelewe ni kwa nini uliamua upande wa Bwana. Usiorodheshe dhambi zako, hapana, zungumza kitu cha maana kilichofanya ukaamini uwepo wa Mungu.

3. Ongelea suluhu- Talk of the solution. Ukishaeleza dhambi zako na kilichokuvutia kwa Mola, waambie wasikilizaji wako baada ya kumjua Mungu, uliipata suluhu gani na kiaje. Ni muhimu sana ili kuwavutia wasiomjua Mungu na pia wale ambao wako na shida na dhambi kama zako.

3. Sema ukweli- Be honest. Usitoe ushuhuda ili kumfurahisha mtu. Sema maneno ya ukweli ambayo umeyashuhudia mwenyewe. Kuna watu ambao wanapenda tu waonekane mbele ya watu wakiongea lakini wanachokizungumza ni upuzi mtupu. Kama huna uhakika na jambo lolote, liepuke kuliongelea mbele ya uma sababu utawapotosha. Kuwa mkweli.

4. Toa mifano bora- Give relevant examples and stay focused. Wakati wa kutoa ushuhuda, ni muhimu sana utumie mifano. Lakini usitoe bora mifano sababu nimesema utumie mifano, toa mifano bora na inayo ambatana na unachokizungumzia. Pia usiende nje ya mada yako, usiwapotoshe kondoo.

5. Usitumie maneno magumu- Avoid vocabularies. Msikilizaji na mtazamaji huenda sio wa haiba au ngazi yako kimasomo, huenda unayaelewa maneno mazito mazito na ya ndani ya Bibilia ama Koran lakini yeye haelewi. Kwa sababu hii, tumia lugha na maneno mepesi ambayo kila mtu, ndio kila mtu, atakuelewa bila kumpa kibarua.

6. Chunga wakati- Watch your time. Hakuna kitu ambacho huchosha watu kama kuutumia muda wao zaidi ya mlivyoelewana. Hakikisha unautumia muda uliotengewa na ikiwezekana jaribu kupunguza kidogo ili usiwaudhi, usiwabore, watu. Ukipitisha muda, ole wako, hawatukusikia tena. #ASANTE


1 comment:

  1. I really like this, inapendeza sana. God Bless!

    ReplyDelete