Wednesday, 24 February 2016

HOW TO KNOW THE RIGHT PERSON IN LOVE....

7 Ways to tell whether you are in love with the right person 

1. Mtu wa kwanza kufikiria- The first person you think of. Kama kila siku ukirauka asubuhi mtu fulani ndio wa kwanza kuwaza, basi jua kwamba kuna msukumo wa kimapenzi baina yenu. Mtu huyu ukifikiria kumhusu pia unabambika tu na kujawa na raha.
2. Kipaumbele- You prioritize the person first. Kabla ya wewe kuingiwa na hisia za kimapenzi/mahaba, ulikuwa unajipa kipaumbele. Yani ulijiona mtu bora kabisa katika sayari na mambo yako ulitaka kuyatimiza kabla ya wengine lakini ukiona ushaanza kupatia kipaumbele mambo ya mtu mwingine, jua basi hayo ni mapenzi. Ushaanza kuogelea katika bahari la kimahaba.
3. Utafanya Chochote- You will do anything. Ikiwa mtu ambaye mko katika uhusiano naye huwa unamfanyia ama uko tayari kumfanyia chochote ili kumridhisha, na yeye pia atafanya lolote kwa ajili yako, basi bila shaka hapo kuna mapenzi.
4. Hakuna haya/aibu – You aren’t embarrassed when together. Kama ‘mtu wako’ hamhaibiki wakati mko pamoja, basi hayo ni mapenzi sababu kuna mtu ambaye mkiwa naye hata barabarani hutaki akushike mkono sababu labda havai vizuri, sio mrembo/mtanashati yani hana beauty yoyote. Kama mnatambulishana hata hadharani kwa marafiki, dah! mahaba niue.
5. Tabia unazopenda- Qualities you prefer. Kama mwenzako ako labda na zile tabia unazotamani mpenzi wako awe nazo na kila saa ukimwambia anaona kama unamtania, basi jua huyo ndiye. Yaani unaona hakuna mwingine isipokuwa yeye tu! Raha kweli kweli chambilecho Ali Kauleni.
6. Fikra kubwa/ You think big. Ukitaka kujua kabisa kama unaogelea katika bahari la mapenzi, kila mara ukiwaza kuhusu mpenzi wako unaona tu mambo makubwa. Unaanza kupanga akilini jinsi mtakavyo ishi pamoja, wapi mtaishi, nyumba mtaishi, familia kiasi gani NK. Hapo ni mahaba tupu aisee.
7. Mpenzi ni rafiki wa karibu- The person is your closest and best friend. Kama mpenzi wako ndiye rafiki wa karibu kabisa na hakuna siri kubwa kubwa baina yenu, basi huyo ndiye mpenzi. Hisia zako kwake hazina kipimo wala masharti. Wapenzi ni marafiki yani kufa kuzikana. #ASANTE



1 comment:

  1. Walahi Kakamusa utatumaliza,,, great tips man.

    ReplyDelete