1.Tengeneza mazingira mapya- Build an Inner World. Unapohisi umelemewa kabisa ama umeboeka sana,
jaribu kutafuta mazingira mapya. Si maanishi uumbe ulimwengu wako, ah ah! Namaanisha
ujaribu kutafuta mahali tofauti na ulipo wakati umeboeka. Mazingira mapya
katika fikra zako yatasaidia kulipa deni akilini mwako deni ambalo linachangia
kuboeka. Tafuta idea mpya na tofauti.
2. Fanya jambo la dhamana na maana- Seek Quality. Je unachokifanya sasa hivi ni nini? Kinadhamana au
maana yoyote? Ni kitu gani ambacho ni cha dhamana ndani yako? Dhamana ndio kitu
cha muhimu maishani. Wakati umeboeka hakikisha unajiuliza haya maswali na
ukishayajibu, utaondoa kuboeka ndani yako.
3. Kubali hali kisha pambana- Accept
the situation then resist. Huenda una kazi nyingi sana ya kufanya, uko busy. Kubali hali ilivyo
alafu tafuta mbinu za kijanja za kupambana na hali ya kuboeka. Unaeza
ukapumzika kwa dakika kadhaa, break, kunywa kinywaji ukipendacho lakini
sijasema kileo, nhaha.
4. Jifungue minyororo- Unchain
yourself. Uhuru wa
akili ni kitu muhimu sana katika hii sayari ya pekee yenye uhai, Dunia. Usiwe
mtumwa wa kazi ambayo unaifanya, usijilazimishe katika chochote. Taratibu tu
kama taarab na mambo yatakuwa laini kama mstari. #ASANTE.

This comment has been removed by the author.
ReplyDelete