Thursday, 18 February 2016

HOW TO WIN BACK YOUR FRIEND ! Rahisi sanaaa..



 The following are 12 key points that can help bring back your friend..

1.Tafuta chanzo cha kukosana. Ni nini haswa kilichozalisha uhasama na kuchangia kutoelewana kwenu. Tambua chanzo hiki kisha ukabiliane nacho kisawasawa.

2.Usichukulie mzaha. Marafiki ndio hupenda mzaha na kutaniana, lakini wakati unasuluhisha tatizo, weka mzaha kando ndio muelewane.

3.Kuwa tayari kuchukua majukumu na kusamehea. Wajibika kiutu na usahau yaliyopita, kwani ni ndwele? Toa msamaha kama ulikosewa na kama ulikosa pia omba msamaha.

4.Fikiria utakachomwambia mwanzo na mapema. Kabla ya kupanga lini na wapi mtakutana, jipange na lugha utakayotumia. Fikiria maneno ya kuzungumza. Uwe mpambe wa ‘kiswahili’.

5.Mpigie simu na umuombe mkutane. Ukiwa tayari na ‘maneno’, mpigie simu aliyekuwa rafiki yako na umuombe mkutane ili kutafuta na kuleta suluhu ya tatizo lenu.

6.Mwandikie ujumbe, sms, ama barua. Baadhi ya wati huwa na hasira na kisirani, huenda asishike simu yako. Wakati kama huu, mtumie ujumbe.

7.Mwonyeshe maana ya urafiki. Urafiki ni kama dhahabu, una dhamani kubwa. Asiye na rafiki basi duh! Sijui..

8.Sikiliza aliyonayo pia. Mkisha kutana, usiwe unaongea peke yako, mpatie nafasi pia azungumze, ajieleze na afungue aliyonayo. Kuwa makini.

9.Ongelea mabadiliko. Mwonyeshe jinsi ambavyo umebadilisha tabia anazozichukia. Ongelea mambo ya kujenga. 

10.Mpe muda afikirie kuhusu urafiki wenu. Baada ya nyinyi kuzungumza, mwache rafikiyo afikirie na awaze kuhusu maelewano yenu.

11.Kuwa na subira. Usiwe na pupa. Haraka haina baraka na pia mwenye pupa haadiriki kuvila vitamu. Vijana wa mjini wanasema, ‘kuwa mpole’. Ukitaka heri, basi subiri.

12.Weka mipango na mikakati maalum ya urafiki. Mkishaelewana, wenga mipango ya ni vipi mtaishi na kuudumisha urafiki wenu. Usikubali tena urafiki uyumbe kama mawimbi ya bahari. Kuwa shupavu na ngangari.  #ASANTE

4 comments:

  1. Nhaha noma sana. What a great idea there, longing for more...

    ReplyDelete
    Replies
    1. Good Read,..KakaMusa

      Delete
    2. Shukrani Bingwa. Mwelekeo mwema umechukua. Naomba uwe ukinitumia Barua pepe khaemba80@gmail.com kila unapochapisha bango. Asante

      Delete